Unordered List

Definition List

Aunt Ezekiel Kuhamia Dubai Hadi Kuchopekwa Ujauzito


Mwigizaji nguli katika tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel anadaiwa kuanza kusaka mtoto ikiwa ni miaka miwili tangu afunge ndoa na Sunday Dimonte.

Hii ni baada ya siku chache zilizopita alipofunguka kuwa miaka yake ya kupata mtoto ni sasa ama sasa hivi.

Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Aunt, siku si nyingi staa huyo atakwenda kuweka makazi ya muda kwa mumewe Dubai hadi atakapopata ujauzito.

Akizungumza na Amani hivi karibuni, rafiki huyo ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe kwa kuogopa kusutwa na ‘matarumbeta’, alisema wengi wanadai mume wa Aunt yuko jela kwa hiyo ili kuwahakikishia kuwa kitu hicho hakipo ameamua aende kuishi Dubai kwa muda hadi atakaponasa ujauzito.

“Kama mipango yake itakwenda vizuri, baada ya Mwezi Mtukufuwa Ramadhani kupita ataondoka na safari hii atakaa sana Dubai hadi Mungu atakapomjalia kupata mimba ndipo atarejea Bongo."

"Lakini baadaye ataondoka tena kwani hata kujifungua amependa akajifungulie Dubai,” alisema rafiki huyo.

Baada ya kupata nyepesinyepesi hizo, Amani lilimtafuta Aunt na kufanikiwa kukutana naye uso kwa uso alipoulizwa alisema hapendi kuweka hadharani mambo yake na mumewe lakini kuhusiana na ishu ya kwenda kuishi Dubai,muda si mrefu ataondoka.

“Nadhani unajua kuwa mke na mume Mungu akiwajalia afya njema ni muhimu ndoa ijibu kwa kupata mtoto, sasa kuhusu kwenda kuishi Dubai ndiyo mipango yangu.
“Nataka kuwakomesha wale wanaodai kuwa mume wangu amefungwa! Sitaki kuwajibu kwa maneno, nataka kuwajibu kwa vitendo,” alitamba Aunt
Aunt Ezekiel Kuhamia Dubai Hadi Kuchopekwa Ujauzito Aunt Ezekiel Kuhamia Dubai Hadi Kuchopekwa Ujauzito Reviewed by Unknown on Thursday, July 24, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.