Unordered List

Definition List

Ndoa Ya Kim Kardashian Na Kanye West Yasimamishwa?!?

Kim Kardashian na Kanye West, Kava Ya Ndoa Yao
Tetesi zinazidi kumiminika kuwa ndoa ya wawili hao inaonekana haitakuwa kweli na hakutakuwa na harusi yeyote.

Kulingana na gazeti la In Touch Weekly, kulinganana na fununu zisizojulikana chanzo chake, ndoa ya Kim na Kanye itasalia ndoto.

Fununu hizo ziliendelea kusema kuwa Kim na Kanye wameendelea kuwa na migogoro isiyotaka kuisha kwa sababu Kanye anataka kumtawala Kim kwa njia zote zile.

Hizo tetesi si mpya kwani ilishabainika kuwa Kanye ameamua kumtumia Kim.

Ingawa katika mahojiano kadhaa katika habari, Kim alisema hakuna wasiwasi Kanye akishughulikia maswala ya ndoa kwani tayari ashaolewa mara mbili.

Lakini tatizo ni kuwa Kim hakujua kama atajiingiza katika makaa ya moto kwa kunyenyekea kwa Kanye.

Haijulikani mambo yataenda vipi kwani Kim tayari ana mtoto wa Kanye, kwa jina North West
Ndoa Ya Kim Kardashian Na Kanye West Yasimamishwa?!? Ndoa Ya Kim Kardashian Na Kanye West Yasimamishwa?!? Reviewed by Admin on Thursday, November 14, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.