Unordered List

Definition List

Director Wa Wema Sepetu Ajitetea Baada Ya Fuska

Baada ya tetesi kuwa mfanyakazi wa Wema Sepetu director Chidi kufutwa kazi baada ya kuhusishwa na fuska ya kutumia gari la Wema kutongozea wanawake, sasa mapya yameanza kuibuka.

Kulingana na mdaku wetu aliyeweza kutupasha stori hii katika blog yetu ni kuwa Chidi Mohamed alisema ya kuwa yeye hakufutwa kazi na alikuwa amejiuzulu kwa sababu ya mambo kadhaa.

Kinachomsikitisha Chidi ni kuwa ilikuwaje mpaka watu wakaanza kumharibia jina kwa mambo ambayo hajayafanya.

Chidi amedai ya kuwa kampuni ya Endless Fame ya Wema ilikuwa haina maendeleo na haina maana yeyote kwake.
Pia sababu nyingine aliitoa kuwa kampuni hio inalipa watu fedha kidogo, jambo ambalo lilimfanya yeye kuiacha hio kazi.

Chidi pia aliendelea kusema kuwa kuna watu kadhaa wamempangia kumharibia jina na wanamhofia yeye asiweze kutoboa maovu yanayoendelea katika kampuni ya Endless Fame.

Chidi alikisiwa kuhusika kwa kutumia kari la Wema Sepetu kama danguro la kutongozea wanawake.

Director Wa Wema Sepetu Ajitetea Baada Ya Fuska Director Wa Wema Sepetu Ajitetea Baada Ya Fuska Reviewed by Admin on Saturday, November 30, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.