Unordered List

Definition List

Lady Gaga Afunguka Kuwa Yeye Huvuta Bangi

Msanii wa nyimbo Applause, Lady Gaga amekiri kuwa yeye hutumia Marijuana kwa jina maarufu Bangi.

Msanii huyu ameongezea kusema kuwa kwa siku moja anaweza kutumia vifurushi 15 vya bangi wakati anapofanya shoo yake.

Msanii huyu akiongea na gazeti la Attitude amedai kuwa yeye alikuwa akivuta bangi ili kujituliza maumivu aliyoyapata wakati alipofanywa upasuaji wa kiuno chake.

Msanii huyu alisema kuwa alikuwa akitumia bangi ili kupunguza maumivu anayoyapata wakati alipokuwa jukwaani. "Nilikuwa nikivuta na kuvuta kisha nalala halafu napanda jukwaani nikishikwa na maumivu nashuka navuta tenda ili kuua makali ya maumivu." aliongezea Gaga wakati wa mahojiano na gazeti hilo.
Lady Gaga afanya shoo akiwa nusu uchi
Lady Gaga akivua nguo wakati alipokuwa akitumbuiza mashabiki wake

Kulingana na utafiti, bangi ni dawa ambayo humfanya mtu kutosikia maumivu mwilini na pia humfanya mtu kutokwa na hisia za kibinadamu. Nashuku jambo la kutumia bangi ndilo linalomfanya msanii huyu kutokuwa na aibu yeyote wakati anapokuwa jukwaani. Hii ndio sababu msanii huyu huchukua fursa ya kufanya shoo akiwa nusu uchi.
Lady Gaga Afunguka Kuwa Yeye Huvuta Bangi Lady Gaga Afunguka Kuwa Yeye Huvuta Bangi Reviewed by Admin on Sunday, November 10, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.