Unordered List

Definition List

Mwanamke Afungwa Baada Ya kuweka Picha Ya Mbwa Wake Facebook

Mama mmoja nchini Bernalillo atiwa mbaroni baada ya kumuweka mbwa wake mdogo mwenye umri wa wiki nane katika bagi na kusambaza facebook kwa njia ya picha.

Mama huyo mwenye miaka 44 alitaka kujifurahisha na mafriend wake kwa kuonyesha vile mbwa huyo alikuwa mdogo sana kiasi cha kuwa angeweza kumuweka ndani ya bahasha.

Jambo hilo lilikera watu fulani katika mtandao wa facebook ambapo mmoja aliweza kuwaarifu polisi kuhusu tukio hilo la ukiukaji wa haki za wanyama.

Mama huyo kwa jina Mary Snell aliweza kushikwa pamoja na mtoto wake wa miaka 21, James Engel na kupelekwa kituoni kulingana na CNN.

Kiukweli mama huyo mwenye miaka zaidi ya 40 alikuwa anafanya nini facebook? na kama kweli ni shabiki wa facebook, nashuku kama alikuwa na mafriends kweli?

Mama huyo aliweza kukubali makosa kuwa alikuwa anafaya tendo ambalo ni makosa lakini maji tayari yashamwagika.

Labda kama angeweka picha za nusu utupu kwa mtandao haingekuwa makosa kwake
Mwanamke Afungwa Baada Ya kuweka Picha Ya Mbwa Wake Facebook Mwanamke Afungwa Baada Ya kuweka Picha Ya Mbwa Wake Facebook Reviewed by BkuHabari Admin on Sunday, November 24, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.