Unordered List

Definition List

Rais Barrack Obama Na Uhuru Kenyatta Wanagawa Tabia Moja. Wazijua?!?

Si siri kuwa kuna mtafaruku kati ya marais hawa wawili tangu Uhuru Kenyatta asawazishwe kuwa rais wa Kenya. Obama kama alivyotarajiwa, alikuwa anahitajika kuwa rafiki mkuu wa Kenyaatta kwani mizizi ya Obama ni Kenya. Lakini kimtazamo, watu hawachukulii hivyo.

Obama ana upingamizi mkuu kwa Uhuru Kenyatta huku akitaka mahakama ya ICC kuchukua mkondo wake kuhusu swala la kimshtaki Kenyatta.

Ijapokuwa siku ya kumuenzi mwendazake Nelson Mandela walipeana mikono, wawili hao ni mahasimu kwa macho ya umma.

Je wazijua tabia zao mfanano?

Ulikuwa wajua kuwa wawili hao wanatumia mikono yao ya kushoto? Obama na Kenyatta hutumia mikono yao ya kushoto kufanyashughuli zao za kila siku(watu waliowainjoy wakati waliposalimiana na mikono ya kulia nchini Afrika Kusini)

Wote ni wavuta sigara. Obama changamoto yake kuu ilikuwa ni kuacha uvutaji wa sigara tangu alipokuwa chuo kikuu na hadi wa sasa hio imekuwa changamoto kuu kwake. Kenyatta ni jambo la kawaida kwake.

Wote walizaliwa mwakam mmoja, 1961, ijapokuwa Obama alizaliwa kwa umaskini na Kenyatta alikuzwa kitajiri.

Chimbuko lao ni Kenya. Baba mzazi Obama, Obama Snr. alikuwa mkenya, mamake alikuwa mmarekani, wazazi wa Kenyatta wote wakenya.

Rais Obama ni rais wa 44 nchini Marekani na Kenyatta ni rais wa 4 nchini Kenya...hapo kuna ulinganishi kiasi pia.
Rais Barrack Obama Na Uhuru Kenyatta Wanagawa Tabia Moja. Wazijua?!? Rais Barrack Obama Na Uhuru Kenyatta Wanagawa Tabia Moja. Wazijua?!? Reviewed by Admin on Monday, December 16, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.