Unordered List

Definition List

MENINA: Siwezi Kutoa Rushwa Ya Ngono

MWANAMUZIKI aliyeibukia kwenye Shindano la Epiq Bongo Star Search 2012, Menina Atick amesema licha ya kusikia kuwepo kwa baadhi ya wanaume wenye nafasi kwenye ‘game’ la muziki ambao huomba rushwa ya ngono kwa wasanii wa kike ili wawatoe, yeye atakomaa na anaamini atasimama.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Menina, ambaye sasa anasumbua na wimbo wake wa Shaghala Baghala alisema anachoamini ni kwamba msanii wa kike mwenye kipaji hata asipotoa rushwa ya ngono, nafasi ya kung’ara anayo, hivyo yeye atakuwa mfano kwa wengine.

“Mimi…nitoe rushwa ya ngono ili nitoke, mh…kwa kweli hiyo haiwezekani, najiamini na sitakubali kuutumia mwili wangu kwa kugawa penzi ili nisimame kwenye muziki, kwanza nitatembea na wangapi,” alihoji msanii huyo.
MENINA: Siwezi Kutoa Rushwa Ya Ngono MENINA: Siwezi Kutoa Rushwa Ya Ngono Reviewed by Admin on Friday, December 27, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.