Unordered List

Definition List

Mistari Aina 10 ambayo Inaboa Na Kuudhi Ya Wanaume

Kila mvulana ambaye ashawahi kutongoza lazima kawaida hutumia mistari ambayo anaiamini na ameishika kwa akili na mara nyingi huitumia mara kwa mara wakati anapomkabili msichana yeyote. Kuna mistari ambayo huteka hisia za mwanamke yeyote pindi anapoisikia lakini siku hizi mistari mingine imetumiwa mno mpaka imepoteza ladha.

Mistari hutumika kuanzisha mazungumzo baina ya watu wawili lakini mistari mingine hupita mipaka na kuonekana kama matusi, kuonyesha kupitwa na wakati ama kuonekana kama mstari wa kishamba.

Mistari ninayoizungumzia hapa ni kama ifuatayo...

"Waiona hii shati? Hebu iguse uone material yake...hii ni material ya kiboyfriend!" Huu ndio moja wa mistri ya kikumbavu ambayo kuna watu wengine wanaitumia. Naona ukitumia mstari huu utahitaji kofi zito.

"Mpenzi naona umechoka sana kwa sababu leo nimekuona mara mbili, ulikuwa ukizunguka katika akili yangu" huu ni mstari uliopitwa na wakati. Halafu kuita watu ambao umekutana nao mara ya kwaza kuwa wapenzi ni ukosefu wa heshima na unafaa kurekebisha. Pia uongo wa kuwa umekutana mtu mara mbili kwa siku ama kusema umemfikiria sana ni ukosaji akili.

"Halo mrembo, nimekuona wewe pekee miongoni mwa wanawake wote hawa, nimekuja hapa kirasmi kukununulia kinywaji" huu mstari si mbaya sana unaweza kutumiwa lakini lazima uujue jinsi ya kuutumia. Ukisema umeona wote lakini nimeangukia kwako inamaana ya kuwa ulijaribu kutongoza wengine wengi lakini hukufaulu. Kwa hivyo lazima umakinike hapa.


"Mambo mrembo? Nakufananisha. Hivi tushawahi kuonana wapi?" Huu ni mstari umetumika sana na umepitwa na wakati. Pia mstari huu utakufanya uonekani muongo.

"Eti wapenda kuangalia soka? Je unaweza kuinama kama vile Beckham??" Hahahah huu ni matari wa mazuzu.

"Hivi uliumia baada ya kuanguka kutoka mbinguni?" Huu umetumiwa sana mpaka ukiambia demu yeyote atatabasamu tu!

"Wazungumza lugha gani? Mimi naongea kifaransa" Kujionyesha kuwa wajua lugha nyingi haiwezi kakufanya uteke hisia za msichana, tumia akili wewe.

pia unawza kusoma:
Mambo 5 Wanaume Hufanya Ambayo Huogopesha Wanawake

"Ingekuwa mimi ningeweka herufi 'U' na 'I' pamoja, kama vile zilivyowekwa katika keyboard" Kama wewe bado watumia huu mstari nenda kanyonye...huu ni utoto mwingi.

"Oya sista! chunga hapo mbele kuna shimo" Kujaribu kuteka umakini wa mwanamke si lazima umtishe na vitu vya kujinga, hebu tafuta mbinu nyingine.

"Naona uko na bakuli mimi niko na kijiko" Kutumia lugha fiche ukidhani hutaeleweka ni ya kazi gani? Gonga ndipo na uache uoga.


Je, umeuona mstari wako hapa? Share hii post kwa marafiki zako wajione hapa na wajirekebishe.

Mistari Aina 10 ambayo Inaboa Na Kuudhi Ya Wanaume Mistari Aina 10 ambayo Inaboa Na Kuudhi Ya Wanaume Reviewed by Admin on Sunday, October 06, 2013 Rating: 5

2 comments:

  1. namna ya kumtongoza mke kwa mara ya kwanza

    ReplyDelete
  2. Nimepatana na Dem cmjui ntaanza wapi na nimalizie wapi
    Reply plzz

    ReplyDelete

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.