Unordered List

Definition List

Wawili Wakamatwa Na Polisi Wakiwa Na Kadi 243 Za ATM

Chato. Jeshi la polisi mkoani Geita nimefanikiwa kuwanasa watu wawili wakimili kadi za ATM 243 wilayani Chato.Wawili hao wamepatikana na kadi hizo za ATM ambazo ni za benki ya NMB kinyume na sheria.

Leonardo Paulo, kamanda wa polisi mkoani Geita aliwaambia wanahabari katika ofisi yake kuwa watu hao walikamatwa juzi saa 7 usiku katika kijiji cha Kitela wilayani Chato.

Kamanda huyo ameendelea kusema kuwa wawili hao wamekamatwa na wanahojiwa ili kuweza kuelezea kwa nini walikuwa wanamiliki kadi hizo ambazo ni kinyume cha sheria.

Kadi hizo zina majina tofauti na majina ya washukiwa. Kamanda huyo aliendelea kusema kuwa washukiwa hao wamefanya tendo ambalo halistahiki kisheria.
Wawili Wakamatwa Na Polisi Wakiwa Na Kadi 243 Za ATM Wawili Wakamatwa Na Polisi Wakiwa Na Kadi 243 Za ATM Reviewed by Admin on Thursday, October 10, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.