Unordered List

Definition List

Mambo 5 Wanaume Hufanya Ambayo Huogopesha Wanawake

Kuna mambo mengi ambayo wanaume kadhaa hujiamini nayo pindi wanapojipatia wanawake. Wanaume hujitahidi sana kuridhisha wanawake zao kwa njia tofauti tofauti. Utapata mwanamume anampeleka msichana 'out' kutembea, wakati mwingine humpigia simu kila wakati kumjulia hali, wengine huhakikisha kuwa wanawake wao hawapati shida na wako nao kila wakati.Wengine hujaribu kuwapeleka wanawake wao valentine hata kama hawajaridhika

Lakini swali ni je, hayo yote unayomfanyia mwanamke wako kweli yanamridhisha?

Ukiona kama wewe ni mtu ambaye kila ukifaulu kutongoza msichana baada ya miezi michane msichana huyo hana shughuli na wewe tena, ama hachukui simu zako, basi ujue kuna mambo ambayo wewe unafanya ambayo hayaridhishi kamwe.

Kulingana na askmen.com, kuna mambo kadhaa ambayo wewe unayafanya na yanawaogopesha wanawake.

#1) Kuwa rahisi kuridhisha.  Ni kawaida wanawake wanapenda sana kuridhishwa na mambo kadha wa kadha lakini usipitishe mipaka. Ukionekana wewe wapenda kumridhisha mpenzi wako sana haswa  miezi ya kwanza kujuana basi ataanza kukushuku kama hauko mkweli na unafanya tu hivyo kumuonyesha.

#2) Kujishungulisha sana na ngono. Mpenzi wako anajua ya kuwa yeye huko hapo kwa ajili yako. Lakini tabia ya kila wakati ukiwa na wewe unafikiria tu ngono basi ujue hufiki popote, atakuona kama unataka kumtumia kwa kujinufaisha wewe mwenyewe.

unaweza kusoma pia:
Mistari aina 10 ya wanaume ambayo inaudhi wanawake

#3) Kuonekana kuwa umezama naye sana. Tabia ya kuonyesha uko na wivu mwingi kiasi cha kuwa hujiskii huru ukimuona akizungumza na majamaa ama hupendi kumuona akitembea na wanaweke wenzake kutakutia taabani. Hata kama unahisi wivu, jaribu usimuonyeshe. Na ukubali anavyofanya.

#4) Kuwa mgumu. Wanawake wanapenda kuona wapenzi wao wanawatosheleza mahitaji yao. Ni kweli kuwa hawawezi kukutegemea 100%, lakini tabia ya mwanamume kumuomba pesa mpezi wake siku za kwanza kupatana inaashiria mengine, utaachwa kwenye kiza.

#5) Kuzungumzia kuhusu uhusiano wako na wapenzi wa zamani. Hakuna mwanamke ataridhika kukaa na mwanamume ambaye kila wakati anaongea kuhusu mpenzi wake wa zamani, ukifanya michezo ukakuwa single maisha yako yote.
Mambo 5 Wanaume Hufanya Ambayo Huogopesha Wanawake Mambo 5 Wanaume Hufanya Ambayo Huogopesha Wanawake Reviewed by Admin on Saturday, October 12, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.