Unordered List

Definition List

JK Awazomea DC Wa Pwani; Acheni Uzembe

Pwani. Rais Jakwaya Kikwete alikatiza kimya chake jana baada ya kuwazomea wakuu wa wilaya na watendakazi wengine katika mkoa wa pwani. "Acheni tabia ya kukaa maofisini na kungojea majarida mezani." alisema raisi.

Rais yuko mkoani Pwani kwa siku sita kwenye ziara ya kutembea na kuweka mawe ya msingi katika miradi ya maendeleo. Kikwete aligadhabishwa na vile viongizi wa mkoa huo wanazembea kazini. Kazi yao kuu ni kungojea matokeo ya miswada. Hawawezi kujua kama miswada inafanyika au imefungwa.

"Kama kuna kiongozi ambaye ameshindwa na kazi yake ni vyema aache madaraka hayo na awapatie wengine wachukue hio nafasi."aliendelea kusema. Kitwete alikuwa akiongea hayo alipokuwa na watendaji mbalimbali mkoani humo.

Mkoa huo wa Pwani unasemekana kuwa miradi mingine inakwamishwa bila ya viongozi hawa kutilia maanani. Rais aliwaomba wakuu hawa watumie hii fursa kutembelea miradi yote inayofanyika na pia kutangamana na wananchi kujua hisia zao kuhusu miradi tofauti tofauti. ""Wakuu wa wilaya lazima muweke mpango wa kila siku na kila mwezi kuwatembelea wananchi wenu mjue matatizo yao na sio tu kukaa maofisini na kusoma majarida...mimi nasema kama wewe ni mkuu wa wilaya na hauna mpango wowote wa maendeleo katika kilimo ni bora urudi kwenu ukalime magimbi acheni kujaza nafasi hali kuna watu wapo nje wanasubiri nafasi hizo, wala siwalazimishi kufanya kazi kama umechoka ondoka." aliwaambia wakuu hao.
JK Awazomea DC Wa Pwani; Acheni Uzembe JK Awazomea DC Wa Pwani; Acheni Uzembe Reviewed by Admin on Friday, October 11, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.