Unordered List

Definition List

Mwandishi Wa Habari Wa ITV & Radio One Ufoo Saro Apigwa Risasi. Mamake Auawa



Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata hivi punde katika habari mpasuko ya Radio One kupitia ujumbe mfupi wa simu za mkononi kwamba, Mwandishi wa habari na Mtangazaji wa ITV na Radio One Stereo Ufoo Saro amejeruhiwa kwa kupigwa risasi baada ya kuvamiwa na mtu asiyefahamika nyumbani kwake Kibamba Kinondoni Jijini Dar es salaam. Aidha mvamizi huyo alimuua mama yake Ufoo papo hapo na yeye mwenyewe kujiua kwa risasi, 
Aidha anayedhaniwa kufanya mauaji hoyo ya kutisha  ni mume au mchumba wa mwandishi wa habari wa ITV na Radio One Ufoo Saro na yeye mwenyewe kujiua.
akizungumza na mtandao huu kamanda wa polisi wa mkoa wa kipolisi wa kinondoni kamanda Wambura amesema tukio hilo limetokea majira ya alfajiri ya leo.
Kamanda wambura ameongeza kuwa mwanaume huyo anafanya kazi umoja wa mataifa UN huko sudani ila bado haijafahamika kwamba anafanyia kitengo gani (japo kwa habari za mtaani zinasema mtu huyo ni mwanajeshi ila bado hazijathibitishwa)
Kamanda Wambura anasema inasemekana kulikua kuna ugomvi kati ya wawili hao ambapo walishindwa kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa mama mzazi wa Ufoo Saro(mama mkwe) na ndipo mwanaume huyo alipomshutumu mama mkwe wake kwamba anamtetea mwanae ndipo alipotoa bastola na kumpiga mama yake na Ufoo Saro Risasi ya kichwa na kumuua papo hapo na kisha akampiga Ufoo Saro risasi ya mbili moja ya tumboni na ingine ya mguuni na kudhani kwamba amemuua kumbe amemjeruhi tu kisha kujipiga mwenyewe risasi ya kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.

Habari hii imedondoshwa kutoka Tuangaze Bongo
Mwandishi Wa Habari Wa ITV & Radio One Ufoo Saro Apigwa Risasi. Mamake Auawa Mwandishi Wa Habari Wa ITV & Radio One Ufoo Saro Apigwa Risasi. Mamake Auawa Reviewed by Admin on Sunday, October 13, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.