Unordered List

Definition List

Ozil: Maisha Ya England Ni Matamu

Ozil alijiunga na team ya Arsenal kutoka Real Madrid kwa euro 50 million mwezi wa Septemba na anaenjoy maisha ya London.

"Najiskia niko na furaha katika team ya Arsenal na najiskia vizuri sana nikiwa hapa;" Ozil aliyatamka haya katika kikao cha wanahabari mjini Cologne.

"Mkufunzi wangu ananiamini na team nzima yote iko na ushirikiano na mimi, jambo hilo tu ndilo muhimu kwangu kwa sasa." alisema.

"Naipenda London, ni mji ambao una mambo mengi ya kupendeza na hata nimeshazoea kuendesha gari kwa upande wa kushoto...nilidhani ingekuwa vigumu lakini kwa usaidizi wa Per Mertesacker kunipa mafundisho ya kupeleka gari huku, imekuwa rahisi kwangu kupeleka gari bila shida"

Changamoto za Ozil kwa sasa ni kuona team yake ya Ujerumani imefuzu katika kombe la 'World Cup'. Ujerumani iko na point tano katika Kundi la C na wanahitaji point moja tu dhidi ya Ireland mjini Cologne ili kuhakikisha wamejiunga na kombe hilo mwaka wa 2014.

"Tumejitayarisha vyema kuhakikisha tumeshinda mechi hii." aliongea Ozil ambaye itakuwa mara yake ya 50 tangu kucheza mechi ya kimataifa. "Tunajua kuwa Ireland hucheza mchezo mgumu toka mwanzo hadi mwisho, lakini naamini tutashianda."
Ozil: Maisha Ya England Ni Matamu Ozil: Maisha Ya England Ni Matamu Reviewed by Admin on Saturday, October 12, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.