Unordered List

Definition List

Muvi Ya Justin Bieber Kuzinduliwa Siku Ya Krismas

Inaonekana wakati huu wayahudi hawatakuwa pekeyao katika mikahawa ya sinema msimu huu wa krismasi. Wataungwa na mafans wa Justin Bieber ulimwenguni mzima.

Justin Bieber leo aliweka wazi kuwa filamu yake itazinduliwa rasmi siku ya Disemba 25. Katika filamu hiyo iliyoendeshwa na Jon M.Chu, kutakuwa na wasanii wengi kama vile Ludacris, Mike Posner, Scooter Braun, Usher na wengineo.

"Nimejawa na furaha kuhusishwa katika filamu hii, na naskia vizuri nikiwarudishia mafans wangu kile wanachokipenda." aliongea Bieber katika hotuba yake.

"Jon Chu na timu yangu nzima tumefanya kazi nzuri kuhakikisha kuwa tumeleta mambo mapya kwa 'Beliebers' wote ulimwenguni. Siwezi kungojea hiyo siku ya krismasi kuona muvi hio ikionyeshwa katika sinema.

Hushinikiza hio filamu yake, Bieber alianzisha #MusicMonday katika mitandao.

Justin Bieber aliahidi kutoa nyimbo mpya kila jumatatu hadi siku hio ya krismas. Nyimbo ambazo tayari ashazitoa zikiwemo 'Heartbreaker' na 'All That Matters'

Wadaku wa hii blog wameamua kuwafurahisha mafans wa Justin Bieber kuwa kila Jumatatu wategee ndani ya hii blog kuskiliza nyimbo mpya ya Justin Bieber, utakuwa wa kwanza!
Muvi Ya Justin Bieber Kuzinduliwa Siku Ya Krismas Muvi Ya Justin Bieber Kuzinduliwa Siku Ya Krismas Reviewed by Admin on Thursday, October 17, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.