Unordered List

Definition List

Wawili Waachiliwa Kwa Dhamana Baada Kupatikana Na Maiti Yenye Mihadarati

Dar es salaam. Polisi wa kitengo cha kudhibiti mihadarati wamewaachilia wawili ambao walikamatwa kwa madai ya kuwa na maiti yenye mihadarati tumboni. Polisi mkuu wa kitengo hicho, Godfrey Nzowa aliiambia Mwananchi kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kudhibitisha ya kuwa wawili hao walikusudia kitendo hicho au la.

Nzowa aliliambia gazeti la Mwananchi kuwa wawili hao wako huru lakini kukipatikana ushahidi wowote wa kuwahusisha basi watafunguliwa mashtaka kirasmi.

Jambo la mihadarati linakisiwa huharibu maisha ya wengi na serikali imechukua hatua ya kuhakikisha ya kuwa wameangamiza mihadarati yote.

Tukio hilo lilifanyika Septemba 22 maeneo ya Tabata ambapo mwendazake aliyejulikana kama Rajab Kidunda (43) alipatikana ameaga dunia katika mazingira ya kutatanisha akiwa amelala katika godoro lililoezekwa sebuleni.

Inadaiwa mwendazake alikuwa mgonjwa alipofika nyumbani humo alipotoka kuchukuliwa kutoka Mtwara na kuletwa Dar es salaam.

Polisi baada ya kupashwa jambo hilo waliifikisha maiti hiyo hadi hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa upasuaji. Hapo ndipo aligunduliwa kuwa na pipi 33 aina ya Heroin zenye uzani wa gramu 561.

Mmoja wa wahutumiwa hao ni bibi ya mwendazake na polisi wamewapatia wawili hao masharti kuwa wawe wakiripoti kituoni kwa muda waliopewa huku polisi wakiendelea na uchunguzi wao.
Wawili Waachiliwa Kwa Dhamana Baada Kupatikana Na Maiti Yenye Mihadarati Wawili Waachiliwa Kwa Dhamana Baada Kupatikana Na Maiti Yenye Mihadarati Reviewed by Admin on Thursday, October 10, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.