Unordered List

Definition List

Kim Na Kanye Wanataka Mkataba Kabla Ya Ndoa...

Kwa muda wa wiki mbili mfululizo, Kim na Kanye wamemulikwa sana na vyombo vya habari na kila siku kuna mapya ambayo yanajiri kuhusu wawili hao.

Baada ya Kim kumkubali Kanye kumuoa, sasa mapya yamejitokeza. Kim na Kanye wameandika mkataba wa ndoa.

Mkataba huo unaojulikana kama 'Prenup' ni mkataba ambao hufanywa kabla ndoa na makubaliano nikujua jinsi mtakavyoishi, jinsi mtakavyogawa majukumu na mali wakati wa ndoa na baada ya kuachana.

Wawili hao wamejitosa katika ndoa na tetesi zinasemekana kuwa ndoa yao iko karibu sana kufanyika - tunaingia katika mkataba wa ndoa kwa sababu tunajua ndoa ni jambo la kuogofya.

Kim alieleza kuwa babake marehemu Robert Kardashian kila wakati alimueleza umuhimu wa kuingia katika mkataba wa ndoa.

Wewe wadhani ndoa yao itadumu kweli?
Kim Na Kanye Wanataka Mkataba Kabla Ya Ndoa... Kim Na Kanye Wanataka Mkataba Kabla Ya Ndoa... Reviewed by Admin on Saturday, October 26, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.