Unordered List

Definition List

Rihanna Azuru Abu Dhabi, Afuata Sheria Za Huko

Msanii huyu anayeenziwa ulimwenguni mzima alizuru himaya ya UAE na kuweza kuonyesha ubabe wake kwa kuimba kwa saitu inayoweza kumtoa nyoka pangoni.

Tarehe 10 Oktoba Jumamosi, msanii huyu mwenye asili ya kibarbadian aliweza kuwatumbuiza mafans katika uwanja wa du Arena, Abu Dhabi.

Maelfu ya mashabiki walitumbuizwa kwa mtindo huku Robyn Rihanna Fenty akidondosha nyimbo kutoka albamu ya 'Unapologetic' na nyimbo nyingine zilizoweza kushamiri.

Rihanna yupo katika ziara ya 'Diamonds World Tour' ambapo anatarajiwa kuzuru nchi kadhaa ulimwengu. Kabla kuzuru UAE alikuwa Jo'Berg nchini Afrika Kusini.


Msanii huyu pia aliweza kuzuru Sheikh Zayed Grand Mosque na Yas Waterworld kabla hajafanya shoo yake Abu Dhabi.

Kufuatilia itikadi za kiarabu, msanii huyu wa umri wa miaka 25 alionekana akivalia nguo la buibui nje ya msikiti wa Grand Mosque huku akipozi kupigwa picha.

Cheki picha alizozituma katika mtandao wa Instagram
Habari zinazotufikia ni kuwa msanii huyu alibumburushwa baada ya kukiuka maadili ya kuvaa nguo zilizombana. Rihanna alikataa kusema chochote katika mtandao wa twitter baada ya mashambulizi makali kwa mtandao huo.


Rihanna Azuru Abu Dhabi, Afuata Sheria Za Huko Rihanna Azuru Abu Dhabi, Afuata Sheria Za Huko Reviewed by Admin on Monday, October 21, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.