Unordered List

Definition List

Kesi Ya Papaa Msofe Yapamba Moto Kortini

Kesi inayomkabilki mfanyabiashara maarufu Marijan Abubakar kwa jina lingine Papaa inaendelea. Upande wa Jamhuri umedai kutuma maombi  kwa Wizara ya ya mambo ya nje kukamata wahutumiwa wengine amboyo wako nje ya mipaka ya Tanzania.

Pia maombi hayo yametumwa katika shirika la ujasusi la kimataifa, Interpol ili kuleta watumiwa wengine kizimbani.

Maombi hayo yaliwekwa hadharani Jumatano na wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka katika mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya hakimu mkazi Hellen Liwa. Anaeleza kuwa upelelezi bado unaendelea.

Katika kesi hii Papaa Msofe pamoja na mwenzake Makongoro Nyerere wanahutumia kumuua Onesphory Kituli kimaksudi. Kesi hii ilihairishwa hadi Oktoba 23 mwaka huu ili uamuzi wa maombi ya utetezi ya kutaka kufutiliwa mbali kesi hiyo kutokana na kesi hiyo kuchukua muda mrefu bila kutatuliwa. Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda jambo hilo tarehe 11 Oktober, 2011.
Kesi Ya Papaa Msofe Yapamba Moto Kortini Kesi Ya Papaa Msofe Yapamba Moto Kortini Reviewed by Admin on Thursday, October 10, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.