Unordered List

Definition List

Wema Sepetu: Sigara Hunitoa Mawazo

Katika wasanii wote nchini Tanzania, Wema Sepetu ndiye ameweza kugonga vichwa vya wengi huku akihakikisha umaarufu wake unazidi kuendelea na kuimarika.

Kila akifanya jambo ama kusema kitu, mafans wake wako tayari kufuatilia.

Star huyu amekolea sana kwa ulingo wa filamu za kibongo la kila anapotoa filamu yeyote lazima mashabiki wake huwa tayari kuziangalia.

Hivi majuzi alikuwa na mgongano wa kimapenzi na mpezi wake wa zamani Diamond na hadi sasa haijulikani kama wapo pamoja ama wameachana.

Hivi majuzi alipopiga picha akiwa amevalia viatu vya Diamond alizua hisia kwa mafans wake na wengi wameashiria kuna kitu kisichobainika kati ya Wema na Diamond. Mamake ijapokuwa amelaani mahusiano ya wawili hao.

Katika kipindi chake cha 'In My Shoes' kinachopeperushwa na runinga ya East Africa, Wema amewafungulia moyo mafans wake na kukiri kuwa yeye hutumia sigara ili kupunguza fikra na mawazo. "Mimi huwa navuta sigara pindi ninapokuwa na mawazo, nikivuta huwa inanisaidia kupunguza na kunifanya niwe vizuri." alikiri hayo.

Uvutaji wa sigara si jambo geni kwani wengine huamini kuwa inasaidia kutuliza mapigo ya moyo. Haya endelea dada bora tu usiyachafue mapafu yako.

Wema Sepetu: Sigara Hunitoa Mawazo Wema Sepetu: Sigara Hunitoa Mawazo Reviewed by Admin on Saturday, October 19, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.