Unordered List

Definition List

Kuna Dalili Kuwa Rihanna Atarudiana Na Chris Brown??

Chris Brown hivi majuzi aliweza kuachana na mpenzi wake mpya Karrueche Tran. Inasemekana wawili hao walikuwa na migogoro mingi na siku ya Oktoba 21 waliachana kirasmi. Je, Rihanna ataitumia nafasi hiyo kurudiana na Chris Brown?

Rihanna na Chris Brown wameachana kwa muda mrefu na mara kwa mara wasanii hao hujikuta wamerudiana.Kulingana na rafiki wa karibu wa Rihanna aliyekuwa akihojiwa na Hollywood Life, amesema wakati huu ni tofauti.

Je, Rihanna atarudiana na Chris Brown?

Kamwe hawatowahi kurudiana tena, duru zinazoaminika zinasema kuwa uhusiano wa Rihanna na Chris umeisha.

Duru zinasema kuwa mahusiano ya wawili hao yaliisha mwezi wa Mei na yaliisha vibaya sana. Rihanna aligundua kuwa uhusiano wake na Chris hauwezekani kwani Brown ana utoto mwingi.

Riri sahizi ameamua kujishughulisha na muziki wake.

Uhusiano wa Chris na Karrueche bado upo kulingana na duru nyingine huku ikikisiwa kuwa ni ugomvi wa kawaida.
Kuna Dalili Kuwa Rihanna Atarudiana Na Chris Brown?? Kuna Dalili Kuwa Rihanna Atarudiana Na Chris Brown?? Reviewed by Admin on Sunday, October 27, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.