Unordered List

Definition List

Msanii Akumbwa Na Mauti Kwenye Swimming Pool

Msanii huyu wa nyimbo za kiinjili nchini Uganda alikumbana na mauti siku tatu zilizopita. Inasemekana msanii huyu alikumbana na kifo chake baada ya maji ya kidimbwi cha kuogelea yalipomshinda nguvu.

Msanii huyu kwa jina Mac Elvis alijikita katika mziki wa 'urban gospel' na album yake ya 'Church Boy' ilimfanya yeye kutambulika katika usanii na nyimbo zake zilipendeza wengi.

Msanii huyu alikuwa Tanzania kwa likizo ya kujivinjari kabla kisanga hizo kilipokatiza maisha yake. Inasemekana msanii huyu alimtembelea rafiki yake kwa jina 'lulu' anaeishi Mbeza Beach Africana. Inasemekana mauti yake yalimpata wakati alipoenda kuongelea, jambo ambalo lilikuwa la kawaida kwake.

Nchini Uganda msanii huyu alikuwa producer, mwimbaji na mhubiri wakati mmoja...alikuwa akiingia kwa industry polepole kwa vishindo.

Nyimbo alizopata kuimba zikiwemo; Katikiya, Topowa Game, Oli Nange na Love Him Now.

Maiti yake ilitarajiwa kufika Uganda Oktoba 22

Mungu Aiweke Roho Yake Mahali Pema Peponi
Msanii Akumbwa Na Mauti Kwenye Swimming Pool Msanii Akumbwa Na Mauti Kwenye Swimming Pool Reviewed by Admin on Tuesday, October 22, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.