Unordered List

Definition List

Noorah: Mziki Hauna Faida

Mwanamziki huyu amejitokeza hadharani baada ya muda mrefu kunyamza. Mafans wa mwanamziki huyu walingojea kwa muda mrefu kujua kinachojiri kumhusu yeye na mziki wake.

Akizungumza na DJ Haazu katika kipindi cha Ndundo, Noorah alikiri kuwa muziki hauna faida kwake, ni kama starehe, mziki ni kama vile mtu anavyokwenda bar kuagizia kichwaji kulewa ili kustarehe.

Mwanamziki huyu anajulikana pia kwa jina jingine la utani anafahamika kama BabaStyle. "Mimi siutegemei mziki tena kama utanipa faida kwangu, nimeusotea kwa muda mrefu bila mafanikio." aliiambia MJ Radio."Sina time na mziki, sahizi nashughulika na mambo yanayoendesha maisha yangu."

Noora alidadisi kuwa wasanii nchini wamekuwa wengi na jambo hili limefanya kuwe na mashindano makali huku wanamziki kidogo ndio wanaofanikiwa kimziki.

Noora wasia wake ni kuwa maisha ni malengo, na kama kitu hakina faida na wewe basi hakina maana kwako.
Noorah: Mziki Hauna Faida Noorah: Mziki Hauna Faida Reviewed by Admin on Wednesday, October 16, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.