Unordered List

Definition List

Afisaa Wa Polisi Abaka Msichana Wa Miaka 15, Amuambukiza Virusi

Gulu, Uganda. Afisa wa polisi amejipata mashakani baada ya kumbaka mtoto wa miaka 15. Polisi huyo katika kituo cha Paicho mjini Gulu, alishtakiwa kwa kosa la mumbaka msichana huyo mara kadhaa.

Afisaa huyo kwa jina Oryang alishikwa siku wa Jumatano baada ya wakaazi kuenda kutoa siri hio kwa wazazi wa msichana huyo.

Baada ya msichana huyo kuulizwa, alisema kuwa hii ilikuwa mara ya tatu tangu polisi huyu amfanyie laana hio.

Msemaji wa polisi hao, Patrick Jimmy Okemo amedhibitisha kuwa afisaa huyo ametenda kitendo hicho.

Pia aliongezea kuwa baada ya uchunguzi wa damu uliotolewa kutoka kwa mwadhiriwa huyo, amesemekana kuonekana chembechembe za ugonjwa wa UKIMWI.

Nchini Uganda visa vya ubakaji na matendo ya kinyama yamezidi kuongezeka ikizingatiwa kuwa idadi kubwa ya waganda wameathirika na gonjwa la UKIMWI.
Afisaa Wa Polisi Abaka Msichana Wa Miaka 15, Amuambukiza Virusi Afisaa Wa Polisi Abaka Msichana Wa Miaka 15, Amuambukiza Virusi Reviewed by Admin on Thursday, October 17, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.