Unordered List

Definition List

Sitaolewa Na Mahari, Msanii Irene Paul Aweka Wazi

Vitendo vya wanawake kuona mahari kama kitu kisicho cha lazima unaendelea. Msanii wa filamu za kibongo Irene Paul amejitokeza na kusema wakati wake wa kuolewa hataitisha mahari yeyote kwa mtu yeyote. "Sitaolewa na gharama yeyote." aliongea.

Kulingana na paparazi aliyekuwa akimhoji, Irene alisema kuwa swala la ndoa na mahari ni vitu tofauti kwani mahari hayawezi kugharamikia yote uliyoyapitia kutoka udogoni.

"Kama tumeafikiana kuoana na mchumba wangu sitahitaji mahari kabisa maana kwa upande mwingine naona kama ni kutugeuza kama watumwa sisi wanawake." aliongea msanii huyu mtajika.

Beyonce Ajimwaya Katika Mtandao Wa Tumbrl

Mttindo kama huu ukiendelea basi itakuwa afueni kwa wanaume kwani inajulikana sana kuwa wanawake pamoja na wazazi wao wanapenda kuitisha mahari mengi kutoka kwa wanaume ili kuoza mabinti wao. 
Sitaolewa Na Mahari, Msanii Irene Paul Aweka Wazi Sitaolewa Na Mahari, Msanii Irene Paul Aweka Wazi Reviewed by Admin on Friday, October 25, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.