Unordered List

Definition List

Msanii Wa Nyimbo Titanic Celine Dion Aaga Dunia!?

Mitandao ya kijamii inaeneza uvumi kuwa mwanamziki Celine Dion amefariki.

Celine Dion amekuwa mwathiriwa wa mwisho kuuliwa katika mitandao ya kijamii.

Katika vitumizi viwili katika mtandao wa facebook, vinaeneza uvumi kuwa Celine alipatikana na ajali, moja inadai alifariki na ajali ya ndege, na nyingine inadai kuwa amefariki na ajali ya barabarani. Na iliomba watu waingie katika vitumizi hivyo ili kujua zaidi.

Hizo habari za uongo zimeaminika kuwa chanzo chake kimetokana na runinga ya Fox News na CNN ambazo zilikuwa zikisoma:
'R.I.P Celine Dion 1968 - 2013? and "Her heart will go on? Celine Dion died in a car accident"

Kwa kujitetea runinga ya CNN ilijitoa lawamani na kutaja chanzo cha habari hio kuwa ni Global Associated aka Mediafetcher.

Celine Dion kwa muda mrefu amenyamaza na wakati huu anataka kuzindua album yake mpya ya 'Loved Me Back To Life' inayotarajiwa kutoka Novemba 7.

Uvumi huu kwa hakika utamuezesha msanii huyu kupata mauzo bora katika album hiyo mpya.

Jana aliweza kutoa nyimbo yake mpya 'Incredible' na msanii Ne-Yo ambayo ipo katika albamu hio.
Pata kuisikiliza nyimbo ya 'Incredible' [HAPA]
Msanii Wa Nyimbo Titanic Celine Dion Aaga Dunia!? Msanii Wa Nyimbo Titanic Celine Dion Aaga Dunia!? Reviewed by Admin on Monday, October 28, 2013 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.