Unordered List

Definition List

Mpenzi Wa Flora Mbasha Ashtakiwa Na Kosa La Kumbaka Shemejiye

MUME wa mwimbaji Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha (32),amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam akikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo ya ubakaji.

Mshtakiwa huyo ambaye ni mfanyabiashara na mwimbaji alisomewa mashitaka yake mbele ya Hakimu Mkazi, Wilberforce Luago.

Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga alidai kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo mawili maeneo ya Tabata Kimanga, jijini Dar es Salaam. Katuga alidai katika shtaka la kwanza kuwa, Mei 23, mwaka huu eneo la Tabata Kimanga, Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, kinyume cha sheria huku akijua ni kosa alimuingilia kwa nguvu msichana anayedaiwa kuwa shemeji yake (jina limehifadhiwa).

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Mei 25, mwaka huu eneo laTabata Kimanga, jijini Dar es Salaam, kinyume cha sheria, mshtakiwa aliumuingilia kwa nguvu mfanyakazi wake (jina limehifadhiwa).

Hata hivyo, mshtakiwa alikana mashitaka hayo. Upande wa Jamhuri ulidai kuwa hauna pingamizi la dhamana. Hakimu Luago alitaja masharti yadhamana kwa mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili, mmoja awe mtumishi wa serikali na mwingine kutoka taasisi inayotambulika watakaosaini hatiya dhamana ya Sh. milioni tano.

Mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana hivyo alipelekwa rumande na kesi iliahirishwahadi Juni 19, mwaka huu itakapotajwa. Mbasha akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi alisindikizwa katika basi la Jeshi la Magereza kwa ajiliya kwenda kuanza maisha mapya mahabusu ya Keko, jijini Dar es Salaam.
Mpenzi Wa Flora Mbasha Ashtakiwa Na Kosa La Kumbaka Shemejiye Mpenzi Wa Flora Mbasha Ashtakiwa Na Kosa La Kumbaka Shemejiye Reviewed by Admin on Wednesday, June 18, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.