Unordered List

Definition List

Jokate Mwegelo Aingia Sokoni Na Kitu Kimpya

MWANAMITINDO Jokate Mwegelo ameibuka na ubunifu mpya wa sabuni ya kuogea inayokwenda kwa jina la Mo. Hii ikiwa ni baada ya kutesa na bidhaa ya ndala.

Akipiga stori na Risasi Mchanganyiko, Jokate alisema uzinduzi wa sabuni hiyo unatarajiwa kufanyika leo Jumatano, Juni 18, mwaka huu ambapo yeye na timu yake watatembea kwa miguu kutokea mjini (Posta) kuelekea Mbagala huku wakigawa zawadi kwa akina mama.

“Nashukuru nimeweza kubuni tena bidhaa nyingine, nataka kuwaambia wasichana wenzangu, wasilale. Tukitaka tunaweza kufanya makubwa. Nawashauri wapenzi wangu wakae barabarani kunisubiria nitapita na kundi langu la Kidoti ili niwapatie zawadi,” alisema Jokate.
Jokate Mwegelo Aingia Sokoni Na Kitu Kimpya Jokate Mwegelo Aingia Sokoni Na Kitu Kimpya Reviewed by Admin on Wednesday, June 18, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.