Unordered List

Definition List

Shamsa Ford: Siwezi Kuogopa Shepu Yangu Kupotea Sababu Ya Kuzaa Watoto 7

Staa wa filamu za Bongo Movies ambaye pia ni mama amefunguka kuwa anataka kuzaa watoto mpaka aambiwe hospitalini kuwa ametimiza kiwango cha mwisho cha kujifungua.


Akiongea na mdadisi wa karibu na nyota huyu, Shamsa Ford aliweka wazi kuwa yeye hatoridhika kamwa na kuwa na mtoto mmoja. "Tangu tulipoanza uhusiano na mpenzi wangu aitwae Dick, na kujifungua mtoto wa kwanza, tumpepanga kuzaa watoto wengi, kama saba hivi." Shamsa alifunguka.

Alipojaribu kuulizwa na chanzo kama hawezi kuogopa kupoteza shepu lake la umbo, hivi ndivyo alivyosema “Siwezi kutosheka kuzaa watoto wawili au watatu, nitakachofanya nitazaa mpaka basi. Sijali kwamba eti nikizaa nitachuja na kuharibu umbo langu kwani naamini kuwa hata kama nisipozaa bado umri utazidi kwenda na nitakapofikia kuzeeka nitazeeka bila kuwa na watoto,” alisema Shamsa.

Wakubaliana na haya maneno?
Shamsa Ford: Siwezi Kuogopa Shepu Yangu Kupotea Sababu Ya Kuzaa Watoto 7 Shamsa Ford: Siwezi Kuogopa Shepu Yangu Kupotea Sababu Ya Kuzaa Watoto 7 Reviewed by Admin on Thursday, November 20, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.