Unordered List

Definition List

Victoria Kimani: Hakuna Kitu Kama Illuminati Wala Freemason

Victoria Kimani, mwimbaji aliye chini ya usimamizi wa Chocolate City yenye makao makuu nchini Nigeria ameeleza kile anachoamini kuhusu uwepo wa freemason au Illuminati kwenye muziki muziki wa Kenya na imani yake kuhusu suala hilo.

Huku wasanii kadhaa nchini Kenya wakiaminika kuwa ni wafuasi wa Illuminati kama vile Kidis The Jembez, Octopizzo, Jaguar na wengine wengi, Victoria Kimani anapinga madai haya yote.

“Ngoja niwaambie kitu, sidhani kama kuna kitu kama Illuminati au vyovyote vile ilivyo. Sidhani watakuja Kenya na kuwachukua wasanii wetu kwa sababu hatuna hata twitter verification. Hatuna hata video za nyimbo zilizohit zaidi ya milioni kwenye YouTube. Kwa hiyo sidhani kama niko kule lakini ninawa-apreciate kwa kunifikiria kwenye fikra zenu za timu ya illuminate. Mimi sio sehemu ya shirika ama jamii yoyote ya ‘secret society’.” Victoria Kimani ameuambia mtandao wa Ghafla wa Kenya.

Soma: Mkono Wa Shetani Ndani Ya Tusker Project Fame

Ameongeza kuwa yeye ni mwanamuziki ambaye yuko chini ya Chocolate City ambao wana imani ya Kikristo na endapo akijaribu kufanya kitu kama hicho wangemzingua.
Victoria Kimani: Hakuna Kitu Kama Illuminati Wala Freemason Victoria Kimani: Hakuna Kitu Kama Illuminati Wala Freemason Reviewed by Admin on Friday, March 28, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.