Unordered List

Definition List

Diamond Platinumz Aitisha Tsh 80 Milioni Kupiga Shoo Kenya

Msanii wa nyimbo za Bongo Flava Nasib Abdul aka Diamond Platinumz ametishaa.

Hivi karibuni staa huyu anayewika na style mpya ya kucheza ya ngololo amewatisha maorganiser baada ya kudai kuwa yeye si msanii wa hivi hivi na kama mtu anataka kumkodi basi awe na hicho kiwango cha pesa.

Kulingana na habari kutoka gazeti la udaku la Pulse, linadai kuwa Diamond kama unataka kumkodi lazima uwe na hicho kiwango cha pesa Ksh 4 milioni. Kando na kuwa na hicho kiwango, Diamond pia ana gharama nyingine kama vile:
  • Lazima umpe tiketi ya ndege ya first class
  • Tiketi za madansa wake saba
  • Umkodishie hoteli ya 5 stars
Jambo hili limewazuia baadhi ya maorganiser nchini Kenya kumkodi Diamond kufanya shoo na wao.

Hii inachangiwa na kuwa Diamond Platinumz amekuwa akiwika na hivi karibuni amekuwa akifanya kolabo na wasanii wa kimataifa.

Hivi unakualiana na Diamond kuitisha kiwango hiki kukubwa cha pesa ikizingatiwa kuwa Diamond shoo zake huwa si live na anategemea nyimbo kufanywa kupitia kwa DJ na CD.
Diamond Platinumz Aitisha Tsh 80 Milioni Kupiga Shoo Kenya Diamond Platinumz Aitisha Tsh 80 Milioni Kupiga Shoo Kenya Reviewed by BkuHabari Admin on Friday, May 23, 2014 Rating: 5

No comments:

Tunapenda kuyasoma maoni/reaction kutoka kwako!

Kama una maoni tofauti na chapisho la hapo juu, wasiliana nasi kupitia ukurasa wetu wa mawasiliano

Powered by Blogger.